๐ฒ๐ฐ๐ฑ๐ฐ๐ฑ๐ฐ ๐ช๐ฏ๐จ ๐ฌ๐ณ๐พ๐จ๐ฒ๐จ๐ต๐จ ๐ช๐ฏ๐จ๐ต๐ฎโ๐จ๐จ ๐ฒ๐พ๐จ ๐ผ๐ด๐ฌ๐ด๐ฌ ๐พ๐จ ๐ฉ๐จ๐น๐จ๐บ๐จ.
๐๐ฃ๐ฎ๐ฆ๐๐, ๐๐๐ง๐ฎ๐๐ซ๐ข ๐, ๐๐๐๐.
Leo, wanakijiji wa Elwakana, Bumwende, Kaunti ndogo ya Mumias Mashariki, wamejawa na furaha baada ya Gavana Mchapakazi FCPA Fernandes Barasa kutimiza ahadi yake ya kampeni kwa kuwaletea transfoma yenye uwezo wa kusambaza umeme pia katika maeneo jirani.
Akizungumza wakati wa hafla ya kuzinduwa rasmi umeme huo kwa wananchi, Gavana Barasa alifichua kwamba aliamua kuwasha mwangaza huo mwenyewe kama ishara ya shukrani kwa wananchi na wanakijiji hao, ambao wamekosa umeme kwa miaka mingi.
Mwaka jana, Gavana Barasa, akiwa katika jitihada za kuzalisha nishati Kakamega nzima, alikutana na wasimamizi wa kampuni ya uzalishaji umeme kupitia teknolojia ya nishati mbadala, inayojulikana kama โHydrobox.โ Kampuni hii itazalisha umeme katika Jimbo la Kakamega, hususan maeneo yenye mito.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na Wawakilishi wa Wadi wakiongozwa na Mhe. Timothy Anzetse (mwenyeji), Maafisa wa Kaunti wakiwemo Mawaziri, Maafisa Wakuu, Watawala wa serikali kuu na kaunti, pamoja na wananchi.